Mbosso- Nyimbo Zangu Hazipigwi Redioni

Msanii wa Muziki wa Bongo fleva kutoka label ya WCB Maromboso au maarufu kama Mbosso ameongelea Kitendo Cha nyimbo zake kutopigwa na baadhi ya media.

Mkurugenzi wa WCB Diamond Platnumz amekuwa kwenye mgogoro na baadhi ya vyombo vya habari hadi kupelekea nyimbo zake kufungiwa na vituo hivyo.

download latest music    

Wasanii wote ambao wako chini ya WCB wamekuwa wakibaniwa nyimbo zao kupigwa Kwenye Media hizo na Mbosso akiwa mmoja kati ya wasanii hao.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Bongo 5, Mbosso ameweka wazi kuwa ingawa  nyimbo zake hazipigwi na baadhi ya media lakini anashukuru zinadai kila vyema kwa mashabiki zake.

Ukizungumzia moja ya wasanii ambao hawakupata bahati ya kupata nafasi kubwa kwenye radio station, mimi pia naweza kusema nipo.

Sikupata bahati kabisa nyimbo kupigwa kwenye radio station lakini wananchi wamenipokea, wamesema Mbosso tunakusapoti, wamenisapoti nashuru leo nimefika nilipofika”.

Baada ya media zaidi ya nne kugoma kupiga nyimbo za Diamond na wasanii wote wa WCB, Diamond alifikia uwaumuzi wa kufungua Stesheni yao ya Wasafi Tv.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.