Mbosso- Ujana Ulinipelekea Kupata Watoto Katika Umri Mdogo

Msanii wa Muziki wa Bongo fleva kutoka katika label ya WCB, Maromboso au maarufu kama Mbosso amekiri kuwa na watoto wawili katika umri mdogo ni matokeo ya balehe.

Mbosso ambaye kwa hivi sasa anaendelea kufanya vizuri na ngoma yake ya “Nadekezwa” ni Baba wa watoto wawili ambao watoto wote wana umri sawa lakini ni mama tofauti.

download latest music    
Kwenye mahojiano aliyofanya na Bongo 5, Mbosso amekiri kuwa pamoja na kila mmoja kuwa na mama yake lakini hana uhusiano na kama zao kwa sasa kila mmoja ameshaolewa.

Sipendi kuwa muongo na sitakuwa na dhambi ya uongo, huwa inatokea katika ukuaji (balehe) hususani sisi watoto wa kiume, kuna vitu utajizuia navyo lakini hutashindwa tu.

Kwa hiyo sitaki kuwa muongo, ilitokea ikawa hivyo nimekuwa baba nina watoto wangu wawili, tunaishi vizuri“.

Mbosso alianza muziki katika umri mdogo baada ya kujiunga Kwenye kundi la muziki la Yamoto Band miaka kadhaa iliyopita.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.