Mbosso Wa Mkubwa na Wanawe Asainiwa chini ya Label ya Diamond

Mwanamuziki Marombosso au maarufu kama Mbosso wa Mkubwa na wanawe amekula shavu la maana baada ya kusainiwa chini ya label maarufu Wasafi Classic (WCB) Iliyo chini ya mwanamuziki Diamond Platnumz.

Ikiwa Leo ni siku yake ya kuzaliwa ya Mbosso Raisi wa label hiyo ya Wasafi Diamond alitumia fursa hiyo kutangaza habari hii ambapo aliandika;

download latest music    

“Happy birthday Mbosso words can’t express how big of fan of hours I am i can’t wait to officially introduce you as a member of WCB I can’t wait for the world to hear the special and unique talent that you have that makes me be your number one fan, Kheri ya kuzaliwa mbosso maneno kamwe hayatoweza kutosha kukueleza ni kwa kiasi gani mimi ni shabiki wako…Heshima na busara hunifunza mengi nasubiri kwa hamu siku ya utambulisho wako rasmi kama msanii na mwanafamilia wa WCB, Vilevile ulimwengu upate kusikia kipaji kingine kutoka Tanzania. Mwenyezi Mungu akupe maisha marefu Upendo na furaha”.

Mbosso ataungana na wasanii walio ndani ya WCB Kama Mr. lavalava, Harmonize, Rich Mavoko, RayVanny, na wengineo wengi.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.