Mdogo wa Billnas Afunguka Kuhusu Mstari wa ‘Tag Ubavu’ Unaomkana Baba YaO
Mdogo wake na Billnass ambae walishare baba mmoja amefunguka na kuzungumzia huzuni yake na baba yake pia hasa baada ya kusikia wimbo wa tag ubavu ambao kuna mstari katika wimbo huo unaelezea kuwa billnass hamjui baba yake na wala hataki kusikia stori zake.
Katika wimbo wa tag ubavu kuna sehemu inayosema “DINGI HAMJUI NA HATA SRORI ZAKE HAZIKUSUMBUI’ , Mstari ambao umeibua stori na huzuni kwa familia yak kwa sababu hata kama kweli baba wa billnass hakuhusika katika kumlea billnass lakini kuna baadhi ya maswala yanabaki kuwa ya kifamilia.
Steve ambae ni dogo wake na Billnass anamhoji kaka yake alijisikiaje kuimba sehemu hiyo huku akijua kabisa baba yake yuko hai na kwamba hata kama baba hakumlea lakini bado hakupswa kuongea hivyo kwa sababu kuna siri zingine za familia huwa zinabaki katika familia tu, hivyo katika ukurasa wake wa instagram aliandika:-
loh Billnas sijajua kama uliwaza baba atajisikiaje pindi ulipouwa ukiandika na kurekodi dingi haumjui na hata stori zake hazikusumbui,wengi sana wapona tunajua kuwa hawajalelewa na baba zao lakini walibaki kuwaheshimu kwa sababu ukweli wa nani ni mkosaji kati ya baba na mama ni siri yao wazazi hivyo inabaki kuwa hivyo na sio vyema kuwakashfu wazazi , maana atabaki tu kuwa baba yako hata kama utamzidi kwa kipato au elimu bila kujali amekutunza au hajakutunza kiukweli mzee ameumia sana na hajapenda lakini tukuombee tu kwenye muziki wako.