Meneja Ajikanyaga Kuhusu Ugonjwa wa Wema Sepetu

Meneja wa staa wa Bongo movie Wema Sepetu anayejulikana kama Neema Ndepanya amejikuta akikosa cha kujibu baada ya kuulizwa kuhusu hali ya kiafya ya Wema Sepetu.

Siku za hivi karibuni kumekuwa na tetesi nyingi Kwenye mitandao ya kijamii zinazodai Wema alienda nchini India wiki chache kwa ajili ya kukatwa utumbo.

download latest music    

Wema na uongozi wake walikataa tetesi hizo na kusisitiza kuwa yeye ni mzima wa afya lakini taarifa hiyo imeingia doa baada ya video yake ikimuonyesha anaumwa hoi hospitali kusambaa mtandaoni.

Baada ya kuvuja kwa video hiyo,Risasi Jumamosi lilimsaka Wema ili kupata ukweli juu ya afya yake lakini kama kawaida yake simu iliita bila kupokelewa na lakini walipompigia Meneja wake alipokea na kujikanyaga na kupata kigugumizi:

Jamani nipo mbele ya watu hapa siwezi kuongelea suala hilo nitakutafuta baadaye tuongee”.

Lakini alipotafutwa hakutaka kuongea tena Lakini pia Mama Wema alipotafutwa alidaiwa kuporomosha matusi ya nguoni bila majibu yoyote.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.