Meneja Wa Mobetto Adai Mteja Wake Hajatetereshwa na Skendo Ya Uchawi

Meneja wa Msanii wa Bongo movie na mwanamitindo Hamisa Mobetto, Beatrice Ndungu amefunguka na kuweka wazi kuwa Hamisa hajatetereshwa na skendo ya uchawi.

Siku ya jana Hamisa Mobetto aligubikwa na skendo nzito mara baada ya voice notes kuvuja zilizothibitisha kuwa alikuwa anafanya maongezi na mganga wa kienyeji.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Bongo 5, Meneja wa Mobetto ameweka wazi kuwa pamoja na kwamba Mteja wake anapitia kipindi kigumu kwa yale yanayoendelea Kwenye mitandao ya kijamii lakini ni mwanamke jasiri na anajua nini anafanya hivyo yuko vizuri kabisa.

Mitandao ya kijamii inakuja na mambo  mengi mengine mazuri na mengine mabaya lakini nahisi kila kitu ni vile utapokea na kujibu kwa sababu maneno hayaishi watu wanaongea lakini cha muhimu ni vile unajionyesha mbele ya watu kwa majibu yako.

 

Hamisa ni mtu mmoja jasiri mpaka kuna vitu ambavyo ni binafsi sana mimi kama meneja siingilii lakini ninachoamini ni msichana jasiri na amepitia vitu vingi sana na hivyo alivyopitia amefika hatua nzuri inayopelekea makumpuni mengi kumtaka kwa ajili ya kutangaza bidhaa zao na kuna vitu vingi zaidi vinakuja”.

Lakini pia Meneja huyo amesema Mobetto amefungua ukurasa mpya na hayo mambo ameshaachana nayo na hivi sasa anaangalia mambo mengine hivyo mashabiki zake wakae mkao wa kula.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.