Meneja Wa Wema Akana Tetesi Za Wema Kukatwa Utumbo

Meneja wa staa wa Bongo movie Wema Sepetu, Neema Ndepenya amekana tetesi zilizoenea Kwenye mitandao ya kijamii kuwa Wema amekatwa utumbo.

Wiki iliyopita Mwanaharakati wa siasa Mtandaoni Mange Kimambi aliuambia uma wa Watanzania Kupitia ukurasa wake wa Instagram kuwa Wema amekatwa utumbo.

download latest music    

Mange alidai kutokana na kuzidiwa na uzito mkubwa (ubonge) Wema alipata ofa ya kwenda nchini India kwenda kukatwa utumbo kwa ajili ya kupunguza kilo.

Kwenye mahojiano na Global Publishers Neema alisema habari hizo zilizozagaa mtandaoni si za kweli bali ni za nia ya kumchafua staa huyo kitu ambacho wao wamekipuuzia.

Unajua kuna habari nyingine unasikia wala kichwa chako hakiwezi kuuma hata kidogo kwa sababu ni za kizushi, Wema alikwenda India kwa matibabu yake binafsi”.

Wema alikwenda nchini India hivi karibuni na kuzua gumzo baada ya kushindwa kuhudhuria kesi yake ya madawa ya kulevya katika Mahakama ya Kisutu jijini Dar na ndipo ilipotoka taarifa ameenda kufanyiwa upasuaji lakini haijajulikana ni upasuaji gani alienda kufanyiwa.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.