Mh Mwakyembe Aagiza Nandy Kukamatwa
Mh Waziri wa habari na michezo, Harrison Mwakyembe ameagiza kukamatwa kwa msanii wa muziki wa kizazi kipya mwanadada Nandy baada ya kusambaa kwa video zake chafu na kufikishwa kituo cha polisi kwa ajili ya mahojiano na uchunguzi zaidi.
Majibu hayo yamekuja baada ya Mh Goodluck Mlingwa mbunge kutoka Morogoro alipouliza ni hatua gani za serikali zimekuwa zikichukuliwa ili kupambana na wasanii wanaweka picha za uchi na matuzi katika mitandao.
Hata hivyo, Mwakyembe amethibitisha kuwa mpaka sasa msanii Diamond Platinumz bado yuko polisi alikofikishwa tangu jana kwa ajili ya mahojiano baaada ya kuvujisha video akiwa na wanawake tofauti akiwa faragha.
Tulitunga sheria mwaka 2010 lakini tulikosa shaeria za kubana wasanii katika maudhui hasa katika upande wa mitandao.tumeshazitunga hizo kanuni na sasa hivi zimeshaanza kufanya kazi.kuna baadhi ya vijana wamekuwa wakifanya uhuni uhni katika mitandao ya kijamii sana na tumeanza kuwafanyia kazi , yupo msanii Diamond Platinumz ambae amefikishwa polisi tangu jana kutokana na kusambaa kwa picha zake chafu, hata hivyo pia binti nandy pia inabidi akamatwe ahojiwe..