“Mimba Yangu Hainizuii Kupiga Kazi Kama Kawaida”-Ruby

Msanii wa muziki wa Bongo fleva ambaye Hivi sasa anafanya vyema na single yake ya ‘Alele’ Helen George ‘Ruby’ amefunguka na kuweka wazi kuwa pamoja na  kwamba ni mjamzito Lakini sio kikwazo kwake kwani anapiga kazi kama kawaida.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Ruby  amefunguka kuwa, kabla hajapata mimba alihisi labda akiipata atashindwa kufanya shughuli zake nyingine, lakini hali imekuwa tofauti kwani anapiga kazi kama kawaida.

Mwanzoni kabla sijapata mimba nilijua nikija kupata, basi sitaweza kufanya chochote, nilidhani labda nitakuwa nachoka sana, lakini namshukuru Mungu hali imekuwa tofauti kwani baada ya kuipata sasa hivi napiga kazi kama kawaida na nitaendelea hadi nitakapojifungua“.

Ruby anategemea kujifungua Mtoto Wake wa kwanza muda wowote kuanzia Hivi sasa ingawa Mpaka leo bado hajamuweka wazi nani baba wa Mtoto wake.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.