Mimi Mars Amefungukia Mahusiano Yake na Diamond

Mwanamuziki wa Bongo fleva Mimi Mars aliye chini ya Mdee Music anayefanya vizuri na ngoma yake ya ‘papara’ amefunguka na kueleza uhusiano alionao na supastaa wa mziki wa Bongo fleva, Diamond Platnumz.

Kumekuwa na taarifa nyingi ambazo zimedai kuwa Mimi Mars ametoka kimapenzi na msanii Diamond Platnumz.

download latest music    

Mimi Mars amekataa kata kata habari hiyo na kuiita ya uongo kwani anajua kwa nini watu walizusha jambo hilo ambapo amedai kuwa kuna video ilisambaa mtandaoni akicheza wimbo wa Diamond baada ya kuona vile wao wakazua yao.

Kwenye Interview aliyofanya na Times Fm kupitia kipindi chao cha The Playlist Mimi mars amefunguka haya zaidi juu ya tuhuma hizo:

Taarifa hizo hazina ukweli kabisa kwanza cha kushangaza wakati nacheza huo wimbo hata sikujua kuwa ni Diamond, nilikuwa nimeenda kwa fundi akawa ameweka mziki akasema hebu cheza kidogo so I was just dancing kwaiyo hakuna ishu yoyote mbaya”.

Mimi Mars ambaye ni mdogo wa msanii Vanessa Mdee anafanya vizuri kwenye gemu na sio kuimba tu lakini pia Mimi ana kipaji cha utangazaji Mc kitu ambacho watu wengi hawakijui.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.