“Mimi na Diamond ni Marafiki Hakuna Kingine Kinachoendelea”- Wema

Muigizaji wa Bongo movie Wema Sepetu amesisitiza na kusema hana uhusiano wowote wa kimapenzi na Diamond zaidi ya urafiki na ukaribu wa kawaida.

Tetesi za wawili hawa kurudiana ziliibuka mwezi uliopita baada ya Wema kuibuka kwenye moja ya party za WCB na kuanza kukumbatiana na Diamond kimahaba kabisa na ishu hii ilizidi kupamba moto baada ya Zari kukiri kumuacha Diamond kisa kumkumbatia Wema.

download latest music    
Diamond na Wema Enzi za mapenzi yao

Tangu sakata hilo Diamond ameshakataa tuhuma hizo na kusema yeye na Wema ni marafiki tu hawana uhusiano mwingine wowote na Wema pia ameibuka na kuthibitisha hilo.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Bongo 5, Wema alifunguka na kusisitiza kuwa yeye na Diamond wamebaki kuwa marafiki wa karibu tu:

Mimi na Diamond ni marafiki ni marafiki wazuri, nadhani kinachowafanya wengi washangae ni kwa sababu mimi na yeye tulikuwa hatuongei kwa muda mrefu tangia tulivyoachana lakini sahivi tumeamua kukua na we decided to just put all those things behind us na maisha yaendelee kwaiyo hakuna cha kushangaza mimi kuongea naye au akinikaribisha kwenye party za WCB lakini kilichowashangaza ni mimi kuenda kwenye partu akaja kunisalimia mimi and Diamond we did not kiss nilimhug I hug my friends”.

Wema ameendelea kusisitiza kuwa yeye na Diamond ni marafiki tu hakuna cha zaidi na mambo aliyofanya na Diamond pale anaweza kufanya na mtu mwingine yoyote ambaye ni rafiki wa kawaida.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.