Mimi na Hamisa sio Marafiki- Zari

Mfanyabiashara maarufu na mzazi mwenza wa msanii Diamond Platnumz Zari the Bosslady ‘Zarinah’ amefunguka na kuweka wazi kuwa yeye na hasimu wake namba moja Hamisa sio marafiki na wala hawawezi kuwa marafiki.

Warembo wao wawili wapo kwenye bifu kali baada ya Hamisa kuzaa na Diamond miezi michache iliyopita. Tangu kipindi cha nyuma kabisa kulikuwa na tetesi za Diamond kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Hamisa kitu ambacho Diamond alikikataa kata kata lakini mara tu baada ya habari za ujauzito kuenea na hatimaye mtoto kuzaliwa Diamond alikiri kumsaliti Zari na kuzaa na Hamisa.

download latest music    

Lakini baadae Zari na Diamond walisameheana na kuendelea na mahusiano yao lakini tangu kipindi hicho Zari na Hamisa wamekuwa maadui na bifu hilo lilidhihirika zaidi wiki iliyopita pale wote wawili walipoandaa party zao siku moja nchini Uganda.

Kwenye interview aliyofanya na Millard Ayo Tv Zari amefunguka kuhusu hali iliyopo sasa na hasimu wake Hamisa Mobetto:

Mimi binafsi sina ugomvi na Hamisa chochote kilichotokea kati yake na Diamond watajuana wenyewe mimi hivyo vitu havinisumbui wala sijali nina maisha yangu nina nina watoto wangu nina kazi zangu nina mambo mengi ya kufanya sawa kina mambo yalitokea kati ya Baba Tiffa na Hamisa lakini natakiwa nijiulize nataka nifike huko? Yaani nimuache mume wangu kwa ajili yake? Hakuna kitu kama hicho lakini mwisho wa siku mwanaume ni mwanaume utampa kila kitu lakini akitoka atatfuta hata mifupa hivyo sina time ya kumuangalia anachepuka na nani sijui. Ila mimi  na Hamisa sio marafiki na hata tukikutana siwezi hata kumsalimie”.

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.