Mimi na Nandy Sio Kikundi Cha Muziki- Aslay

Mwanamuziki mkali wa Bongo fleva Aslay ameibuka na kuweka wazi kuwa yeye na Msani mwenzake Nandy sio wasanii wa kikundi kimoja cha muziki bali wanafanya tu kazi pamoja.

Siku za hivi karibuni Nandy na Aslay wameonekana wakifanya matamasha kadhaa pamoja Ikiwa ni pamoja na Tamasha lao kubwa la Valentine’s Day lilipfanyika mwezi February.

download latest music    

Aslay ameweka wazi kuwa yeye na Nandy sio kikundi ila tu wanaonekana wakifanya shoo kwa pamoja sababu ya nyimbo zao walizotoa kwa pamoja hasa nyimbo yao ya ‘Subalkheri Mpenzi’ inayofanya vizuri kwa hivi sasa.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Bongo 5, Aslay ameeleza ukaribu wake na Nandy ni wakazi tu na sio kama wao ni kundi la muziki ila mashabiki wanavutiwa na ngoma walizofanya pamoja ambazo ni ‘Mahabuba ‘ na ‘Subalkheri Mpenzi’ ndio maana na wanaalikwa katika show pamoja.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.