Mke wa Alikiba Adaiwa Kuwa Mjamzito Baada Ya Picha Hii

Mke wa staa wa Bongo fleva Ali Kiba, Amina Khaleef ameingia Kwenye headlines baada ya kusambaa kwa tetesi kuwa huenda ni mjamzito baada ya picha yake ya hivi karibuni.

Ali Kiba na mke wake kutoka Mombasa Kenya Amina walifunga ndoa Miezi miwili iliyopita na mara moja Kiba taarifa zilisambaa kuwa Ndoa hiyo imeharakishwa kwa sababu Amina ana kibendi.

download latest music    

Tetesi hizo zimezidi kupambana moto mara baada ya picha mpya ambayo ilipostiwa na Ali Kiba mwenyewe alipokuwa anasheherekea birthday ya Meneja wake Seven Mosha.

Kwenye picha hiyo Alikiba na wanafamilia wote wa RockStars 4000 walionekana katika picha ya pamoja inayodaiwa kupigwa nchini Afrika Kusini.

Usemi wa picha moja ni sawa na maneno 1000 ulidhihirika kwani picha hiyo ilizua gumzo. Hivyo hivyo kwenye picha aliyoipost Alikiba akiwa mke wake, Bi. Amina, meneja wake Seven Mosha pamoja na marafiki zake wengine.

Mpaka sasa Ali Kiba na Mke wake hawajathibitisha taarifa za ujauzito huo na inawezekana asiseme kitu kama inabyojulikana kama Ali kiba huwa ni msiri sana Kwenye mambo yake binafsi hawezi kuyaanika Kwenye mitandao ya kijamii.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.