Mke Wangu Hata Akitembea Uchi Sawa tu ;- Rayvanny
Msanii kutoka kundi la WCB Rayvanny amefunguka na kusema kuwa kwa Dunia ya sasa hivi swala la mavazi kwake halina shida sana kwa sababu anajua kuwa Dunia ya sasa hivi mambo ya mavazi kila mtu anachukulia vile anavyoona yeye hivyo hata kama mke wake atavaa nguo za utupu kwake ni sawa tu.
Rayvanny ambae amekuwa akionekana kutulia sana katika swala la mahusiano na mwanamke aliekuwa nae tangu kipindi bado jina lake halijawa kubwa anasema kuwa mavazi hayatasfiri tabia ya mtu kwa sababu kama mtu ana tabia ya uhuni hata akivaa dela au ushungi basi atakuwa hivyo hivyo hawezi kubadilika.
mtu akiwa mhuni hata vae dela au ushungi muda wote kama kupata wanaume atapata tu, na mavazi kwa sasa hayatasfiri tabia ya mtu lakini ni vile tu mtu anavyovutiwa na muonekano wako.Mimi hata siku moja siwezi kumpangia mke wangu avae nguzo za namna gani vyovyote atakavyo vaa fresh tu hata aseme kuwa atatoka utupu mi niko poa.