Mnaukosea Heshima Mziki Wangu Mkinifananisha na Ruby -Nandy

Mwanamuziki wa bongo fleva, Nandy amefunguka na kudai kuwa amechoshwa na kufananishwa na mwanamuziki mwenzie Ruby.

Kwa muda mrefu sasa Ruby na Nandy wamekuwa kwenye aina ya ushindani ambao unatokana na watu kuwafananisha kutokana na aina ya muziki wanaofanya.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Extra Showbiz, Nandy amesema kwa muda mrefu mashabiki wake wamekuwa wakimfananisha na mwanamuziki mwenzake Ruby hivyo amewataka wanao mfananisha na Ruby waache mara moja kwani miziki yao Ina ladha zilizo tofauti sana pia.

Namheshimu Ruby ni mwanamuziki mzuri, lakini kumfananisha na mimi ni kunikosea heshima mziki wangu ladha ya mziki wangu ni tofauti kabisa na Ruby kutokana na utofauti wangu wa mziki ninaofanya na pia kama unaufahamu mziki wa Ruby anaofanya utagundua ni mziki tofauti”.

Alisema Nandy ambaye hakufafanua kwa undani zaidi alimaanisha nini kwa kusema hayo. Ingawa kila mmoja amesema kuwa hana bifu na mwenzake lakini inasemekana ni kama paka na chui yaani hawaivi katika chungu kimoja hata kidogo.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.