Moyo Niliokuwa Nao Mimi Ni Wa Msaada-Mr.Blue

Msanii mkongwe wa bongo fleva ambae ana historia ndefu katika muziki huku akianza muziki katika umri mdogo mpaka sasa ameshakuwa mtu mzima na bado amekuwa akifanya vizuri katika kazi yake, Mr. Blue amefunguka na kusema kuwa yeye ana moyo wa kusaidia sana na mpaka sasa ameshafanya kolabo na wasanii zaidi ya kolabo 600, na bado yuko tayari kuendelea kufanya kolabo ilimradi kukuza muziki na kipaji cha msanii mchanga anaetaka msaada wake.Akiongelea swala ilo na kuhusu yeye kurudia maneno katika baadhi ya kolabo za wasanii Mr.Blue anasema inaweza kutokea bahati mbaya kwa sababu amefanya kolabo nyingi hivyo anaweza kusahahu kama alishawahi kufanya kitu icho kwenye nyimbo nyingine kabla.

“juzi nilikuwa nimekaa nahesabu kolabo nilizofanya tokea nimeanza game,zinafika kolabo mia sita, kuna huyo sijui katokea wapi na huyu na yule,kwaio kurudia sometimes inaatokea maana sijui niliimba kwa nani na nani kwa kuwa kuna ubinadamu pia, hivyo ukiona nimeimba wimbo afu nimerudia baadhi ya maneno ni vizuri tukae mimi na yeye tubadilishe, ila sipendi kumfanyia mtu kitu hasiridhie maana mpaka nimeingiza sauti yangu manake tumekubaliana.ila kama nimekosea hata kidogo ni kesi ya kibinadamu,moyo niliokuwa nao mimi ni wa msaada. Alifunguka Mr. Blue

download latest music    

Hata hivyo katika mahojiano hayo ya eNews ya EATV, Mr. Blue aliombwa kujibu tetesi zinazosambaa kuwa hajawai kurudisha fadhila kwa producer aliwahi kumsaidia na kumtoa kwenye muziki kipindi yuko chini mpaka sasa amekuwa msanii mkubwa lakini hajawahi kurudi kwa Amma G,”hapana mi nakataa G-lover hawezi kusema hivyo,kwa sababu hata akisema hawezi kusema nataka fadhila , nooh namjua G, G mi namwita dady na yeye ndie alienikuza kwenye game, ”

Hata hivyo Mr. blue anasema kuwa pamoja na kuwa Amma G alikuwa anamsaidia lakini hakuwahi kupewa ela na producer huyo hivyo basi kutokana na kipaji chake yeye kuwa special ndio maana alimchagua yeye na kwenda kurekodi, hivyo msanii huyo anasema kuwa producer huyo alikuwa akijilipa kutokana na kipai alichokuwa nacho yeye.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.