Mr. Blue Afungukia Ukimya Wa Darassa

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Herry Samir maarufu kama Mr. Blue amefunguka na kuvunja ukimya juu suala la Darassa.

Darassa amewahi kutoa wimbo ambao ulikuwa wimbo wa Taifa kwani ulioigwa kila kona na kukubalika kila kona anaweza Kuwa ndio msanii pekee kuandika historia hiyo.

download latest music    

Lakini tangu atoe hit Single yake Darassa amekuwa kimya sana jambo lililosababisha maneno kibao kuibuka Kwenye mitandao ya kijamii ikiwemo tetesi za kuwa Msanii huyo amejiingiza Kwenye matumizi ya madawa ya Kulevya.

Mr. Blue ameibuka na kuwataka watu wampe nafasi Darassa ya kupumzika kwani kilichotokea ni kuwa ameamua kupumzika kufanya Muziki kwa sas na Kwenye mahojiano na kituo kimoja cha habari, Mr. Blue alifunguka haya zaidi:

Darassa mwenyewe ameamua kujipa break kwa sababu amefanya kitu kikubwa sana na mimi sidhani kama kuna tatizo lolote pale mtu anapotaka mapumziko kutoka kwenye muziki kwa sababu hata mimi nilishawahi kujipa break baada ya wimbo wangu wa Tabasamu lakini watu waliongea sana na kudai mimi ni teja lakini hii ndio kawaida ya binadamu kuongea kwa sababu wana midomo”.

Darassa ameshawahi kukana tetesi za kuwa yupo kimya kwa sababu yupo rehab na kusisitiza yupo kimya kwa sababu amechukua mapumziko baada ya mwanaye kuzaliwa.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.