Mr. Blue Ajutia Maamuzi Ya Kutoa Albamu

Msanii mkongwe wa muziki wa Bongo fleva Herry Sameer maarufu kama Mr. Blue amefunguka na kusema kuwa hakuna kitu kimemtia hasara kama kutoa Albamu.

Mr. Blue amesema kuwa hajawahi kupata faida kupitia albamu zake cha zaidi ni kwamba hakuna kitu kimemtia hasara kama kutoa albamu zake na kuzipeleka sokoni.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na kipindi cha Enews cha EATV, Mr. Blue alifunguka mambo haya:

Kusema Ukweli albamu hazilipi aisee kwa sababu albamu yangu ya kwanza nilipewa milioni na albamu yangu ya pili nilipata pesa ambayo nilinunua gari tu Lakini sasahivi single moja Lakini unaweza ukapiga mpaka milioni tano”.

Kutoa albamu kwa wasanii ni mafanikio makubwa sana kwani ndipo wanapotengeneza fedha kwa kuusa muziki wao Lakini kwa nchi kama Tanzania imekuwa tofauti kwani wasanii hawatoi kabisa Albamu kwa Kuhofia kupata hasara badala ya faida.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.