Mr. Blue Athibitisha Kukimbilia Afrika Ya Kusini

Mwanamuziki mkongwe wa muziki wa Bongo fleva Kherry Sameer Rajabu maarufu kama Mr. Blue amethibitisha kuwa amekimbilia nchini Afrika ya Kusini kwa ajili kufanya shoo.

Baada ya kutoonekana Bongo kwa muda mrefu hasa kutofanya shoo za ndani kwa muda mrefu Blue ameweka wazi kuwa ameamua kwenda kwa Madiba ili kubadilisha muelekeo kwa muda.

download latest music    

Kwenye mahojiano yake na Global Publishers, Mr Blue anayebamba na Ngoma ya Mbwa Koko alisema kuwa, kuwepo Kwa Madiba kumemfanya kujisikia tofauti na kuonesha hilo, juzikati alipafomu katika Jiji la Durban na kupata shangwe za kutosha kwa mashabiki wanaofutalia muziki wake.

Nipo huku (Kwa Madiba) ikiwa ni muendelezo wa kazi zangu ambazo nimekuwa nikizifanya nje. Kwa sasa nimeamua kuwekeza nguvu zaidi kupiga dili za nje ya Bongo kama ambavyo nilikuwa nafanya ndani. Si vitu vigeni kwangu, lakini kwa sasa nahitaji kuipeleka kazi yangu next level zaidi.”

Wasanii wengi wamekuwa wakibalisha makazi yao ili kuoata nafasi za kupiga kazi zaidi wasanii kama Ray C na Mr. Nice wamehamisha makazi yao nchini Kenya lakini pia Diamond yupo nchini Marekani kwa mwezi mzima kwa ajili ya kupiga Tour yake ya ‘A boy from Tandale’.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.