Mr. Blue- Sina Tatizo na Diamond Ila Kuna Watu Wanataka Tuwe na Bifu

Msanii mkongwe wa Bongo fleva Khery Sameer  maarufu kama Mr. Blue amefunguka na kudai binafsi hana tatizo lolote na staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz bali kuna watu wanataka wawatengenezeee bifu.

Kwa muda mrefu imekuwa ikisemekana kuwa Diamond na Mr Blue wana bifu kutokana na mara kadhaa Mr Blur amesikika akimtupia madongo mazito Msanii huyo.

download latest music    

Lakini juzi Mr. Blue amethibitisha kuwa hana tatizo lolote na Diamond na hata akauposti Wimbo Mpya wa Diamond #Iyena na kuupa promo.

Lakini pia Kwenye Interview aliyofanya na Wasafi Tv, Mr. Blue amefunguka na kuweka wazi kuwa hana tatizo na Diamond kwani alianza kumsapoti tangu akiwa underground:

Ukikaa na Diamond ukamuuliza atakwambia kuwa mimi nimeanza kumpa sapoti tangu mwanzoni Wakati Diamond hajulikani na waandishi wa habari, hajulikani na mtu yoyote.

Hapo inaonyesha wazi kuwa sina chuki na Diamond wala sina tofauti naye yoyote kama ningekuwa na chuki ningemzuia tangu anaanza kutoka hata nyie msingekuwa na kazi”.

Lakini pia Mr Blue aliendelea kufunguka:

Kinachonichekesha kunishangaza ni pale watu wanapooana nimemsapoti akiwa na mafanikio wanataka nianze kumkandia kitu ambacho hakiwezekani. Mimi Diamond ni mdogo wangu wakati anatoka sikuwahi kuwa na bifu naye wala tofauti naye, kuna I wanaotaka kutuingiza katika tatizo mimi na Diamond”.

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.