Mr Nice:Walichokifanya Irene Na Dogo Janja Sio Mfano Wa Kuigwa

Anafahamika tangu zamani kutokana na kazi nzuri aliyoifanya miaka ya nyuma, Lucas Mkenda  maarufu kama Mr .Nice ni msanii mkongwe wa muziki Tanzania ambae alikuwa akifanya vizuri na kuitambulisha vyema Tanzania nje ya Tanzania kwa style yake ya kucheza iliyojulikana kama Takeu style.Style ambayo ilikuwa ikichezwa mpaka na watoto wadogo.Ni wapi msanii huyo  alikuwa hajulikana, kila mtaa kila wakati utasikia nyimbo za msanii  Mr.Nice zikipigwa.

Akiongelea kurudi kwake katika muziki na jinsi wasanii wengine wanavyofanya style yao ya kutumia kiki ili kuweza ku-boost nyimbo zao ziweze kuvuma na kufanya vizuri Mr,Nice anasema kuwa kiki sio nzuri katika muziki kwa sababu unakuta mashabiki wanakuwa wanaamini na kusapoti kitu ulichotaka kukifanya kwa nguvu kubwa alafu baadae inakuja kujulikana kuwa ni kiki tu, akitolea mfano wa ndoa ya Irene Uwoya na DogJ janja iliyofanyika hivi karibuni anasema kuwa watu hao sio mfano wa kuigwa kwa kiki  walioifanya ya kuwafanya mashabiki waamini wamefunga ndoa kumbe sio kweli.

download latest music    

Swala la kiki kwangu halijakaa vizuri kabisa na ninaomba watu wote kwenye jamii walikemee, kwa nguvu zote kwa mfano hii kiki iliyotokea hivi karibuni ya  Irene Uwoya na Dogo Janja kwamba wameoana kumbe hata sio kweli ni kiki tu wala sio jambo zuri.unatumia nguvu nyingi sana kuwaaminisha mashabiki wako kuwa  mmeoana alafu kirahisi tu inakuja kugundulika kuwa sio kweli.Ukweli ni kwamba huo sio mfano mzuri wa kuigwa hata kidogo.

Hata hivyo katika mahojiano na gazeti moja pendwa hapa nchini Mr. Nice aliongezea kwa kumpa ushauri Aslay ambae amekuwa akitoa nyimbo kila kukicha na kumwambia kuwa yeye mwenyewe ndio  anaua soko lake la muziki kwa sababu hawapi muda mashabiki zake kusikilza nyimbo zake kila siku anatoa nyimbo mpya hivyo mashabiki wanakosa muda wa kusikiliza.Ni bora kutulia kuliko kufanya vitu kwa pupa maana haujui kilichokuangusha ni nini.

Lakini pia akiongelea swala ya yeye kuoa , Mr. Nice anasema kuwa kwa sasa hana mpango wa kuoa amejikita kulea familia yake yenye watoto watatu.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.