Mrisho Mpoto Amjia Juu Afande Sele Kisa Kesi Ya Lulu na Mauaji Ya Kanumba

Msanii wa Muziki Tanzania, Mrisho Mpoto ameshindwa kumvumilia msanii mwenzake Afande Sele na kumpa makavu baada ya Afande Sele kudai maiti ya Kanumba ifukuliwe na ichomwe moto kwa sababu ni mbakaji.

Baada ya kifungo cha Lulu siku mbili zilizopita wasanii mbali mbali walikuwa na maoni yao mmoja wapo kati ya watu hao ni mwanamuziki Afande Sele ambaye aliweka wazi hisia zake na kumjia juu Mama Kanumba kwa kitendo chake cha kufurahia Lulu kufungwa huku akisisitiza kuwa Kanumba ni mbakaji ambaye alikuwa anatembea na mtoto mdogo kama Lulu hivyo hastahili kupewa heshima bali ilitakiwa afukuliwe makaburini na kuchomwa moto.

download latest music    

Baada ya Kuongea maneno hayo ambayo yalionekana kutokumfurahisha Mrisho Mpoto alimjia juu Afande Sele na kufunga haya:

Afande Sele wewe ni kaka yangu na mwandishi ambary sijawahi kuacha kuheshimu maandishi yako…..Nimesoma mara 30 maandishi ulioandika kuhusu Kanumba naomba kujua ile barua uliomuandikia Marehemu Kanumba ulitaka imfikie au ulitaka wanaokuja nyuma yake wamfikishie? Ulitaka wanaokuja nyuma yake wajifunze kupitia waraka wako? Mbona nimepata kusikia marehemu halaumiwi kwa kuwa hana uwezo wa kujitetea? Umesema ulikuwepo Sinza kwenye msiba lakini hukutaka kusogea kuzika kwa sababu umesema we we sio mnafki kama Watanzania walioenda kuzik…ikiwa watu wote wangekataa ile maiti ingekuwaje? Nini hasa lengo la movies za kibongo kuziita maigizo yanayokwenda kwenye kanda? Una ugomvi na Bongo movie au uliandika ukiwa Una jazba kidogo? Mimi ndugu yako Mrisho Mpoto”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.