Msanii Awachana Wanawake Wanaojigonga Kwa Diamond

Msanii wa Bongo movie anayejulikana kama Mary Mawigi amewapa makavu live wanawake wote ambao wamekuwa wakijigonga kwa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz.

Mawigi amewatolea povu hilo wanawake hao na kudai Diamond anawachezea na kuishia kuwatumia tu hao wanawake na mwishowe kuonekana kama chombo cha starehe.

download latest music    

Kwenye mahojiano na gazeti Amani, Mawigi alisema kuwa, wanawake ambao wako kwenye uhusiano na Diamond au wanaotamani kuwa naye wanatakiwa kujifunza kuwa mwanaume huyo amekuwa akiwachukulia kama chombo cha starehe na akichoka anachukua mwingine hivyo wasiendelee kumkubali.

Kwani Diamond ana nini cha dhahabu ambacho wanaume wengine hawana hadi wanawake wamgombee kiasi hicho?

Ninawashauri wanawake wenzangu waache kugombea au kulumbana mambo ambayo hayana faida maishani mwao, wasimame, wafanye kazi wao kama wao, maisha yataenda vizuri tu”.

Diamond ambao anajulikana kama sukari ya warembo amekuwa akidaiwa kuwa Kwenye Mahusiano ya kimapenzi na wanawake kadhaa na hata kutamaniwa na wengine wengi.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.