Mtu Kufuatilia Mambo ya Wengine Utakuwa na Kasoro Kubwa Sana.:-Chin Bees
Msanii wa bongo fleva Chin Bees ametoa yake ya moyoni kuhusu tabia ya baadhi ya wabongo kukaa na kuwa wanafatilia mambo ya watu bila kuwa na uhakika nayo na kuanza kuyatangaza hadharani.
Chin bees anasema kuwa hiyo nikasoro kubwa sana kwa sababu kwa hali ya kawaida mtu mwenye maisha ya kawaida huwezi kukaa na kufatilia mambo ya watu na wakati huohuo unakuta hata yale ya kwako yanakuwa bado hayajakaa sawa lakini unakuwa unakosoa ya wenzako.
kama mtu unakuwa kazi yako kufatilia maisha ya wenzako basi wewe unakuwa na kasoro kubwa sana, huwezi kukaa unaongelea mambo ya mtu miwngine wakati wewe mwenyewe ya kwako yanakuwa hayajakaa sawa.
Chin bees anasema kuwa watu wenye tabia hizo waache na kuanza kujifunza kujali yale yanayowahusu tu.