Mume Wa Mama Diamond Kuwajibu Wanaomsema Vibaya

Ikiwa ni muda mchache nyuma tangu mamam mzazi wa msanii mkubwa nchi Diamond Platinumz kuthibitisha kuolewa na mwanaume ambae wengi wamekuwa wakisema kuwa kijana huyo ni mdogo sana kwa mama huyo, mwanaume huyo ameamua kujibu tuhuma hizo ambazo amekuwa akibebeshwa katika mitandao.

Mwanaume huyo anaejulikana kwa jina la Rally na Mama Diamond walionekana katika baadhi ya picha za pamoja wakiwa katika ndege ikisemekana kuwa walikuwa wakielekea Afrika ya Kusini kwa ajili ya honeymoon yao baada ya kufunga ndoa muda wa wiki chache zilizopita.

download latest music    

Hata hivyo mama wa msanii huyo alishawahi kuwajibu watu kuwa mwanaume huyo hana udogo wowote hivyo watu wawaache kama walivyo kwa kuwa wanapendana  ingawa katika mitandao watu wamekuwa wakisema kuwa ni pesa ndio zilizomfanya mwanaume huyo ajiingize kwenye mapenzi na mama Diamond.

Akiandika katika ukurasa wake wa instagram,Rally aliweka picha akiwa na mke wake huyo huku akiandika ujumbe kuwa wanaosema kuwa ana umri mdogo, umri kwake sio shida wanachojali wao ni kuwa wanapendana na hiyo kwao inatosha.

ndoa sio umri ni makubaliano baina ya watu wawili na Allah hutia mkono wake ,mimi sio wa kwanza alianza  mtume S.A.W , Allah atuujalie kwenye maisha yetu mapya @mama dangote #honeymoon #SouthAfrika.

Wawili hao wamekuwa wakioneka wakiweka picha za pamoja wakiwa south afrika waki-enjoy maisha yao baada ya kufunga ndoa.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.