Mwana FA Aingiza Bidhaa Zake Za Bodyspray Sokoni
Msanii mkongwe wa muziki wa Hip hop Bongo Hamis Mwinjuma maarufu kama Mwana Falsafa ‘Mwana FA’ ametangaza kuingiza sokoni bidhaa yake mpya ya Bodyspray.
Mwana FA amegeukia upande wa pili na sasa anaanza kutengeneza pesa kwa kutumia jina lake ambapo amezindua na kuionyesha kwa mara ya kwanza bidhaa yake ya Body Spray iitwayo ‘FYN BY FA”.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Mwana FA ameandika ujumbe huu kuhusiana na bidhaa yake mpya:
Mwana FA ameingia kwenye orodha ya wasanii wengi waliogeukia ujasiriamali na kutoka nje ya muziki kidogo na kutengeneza kipato Kupitia biashara.