Mwana Fa Ampa Shavu Diamond,Ni Kuhusu Wimbo Wa Halellujah

Mwana muziki anaefanya vizuri katika miondoko ya hip hop bongo , ameibuka na kuamsha tena hisia kwa watu baada ya kuisifia nyimbo ya Diamond Platinumz inayojjulikana kwa jina la Halellujah na kusema kuwa Diamond alipatia kufanya kolabo wa watu hao.

Mwana Fa ambae ameseam kuwa yeye ni shabiki wa kundi la MorganHeritage kwa zaidi ya miaka kumi sasa anafurahi na anazidi kuwapenda hasa baada ya kufanya kolabo na Diamond Platinumz.Mwana Fa ambaye kwa sasa anafanya vizuri na project yao ya The Butcher na wimbo wao wa Upo Hapo waliofanya pamoja na Ay na Fid q anasema kuwa kundi ilo limekuwa likifanya vizuri sana tangu zamani na ni kundi ambalo amekuwa na mapenzi nalo kila siku na kitendo cha kuimba na msanii Diamond kinazidi kumfanya azidi kuwapenda wasanii wa kundi hilo.

download latest music    

Akiongea na kipindi cha uhondo cha E fm msanii huyo akusita kuonyesha hisia zake,”MorganHeritage ni kundi nililolisikiliza , sana tena kwa miaka mingi sana tangu 2005/2006 na ninaendelea kuwasikiliza mpaka leo ni takribani miaka kumi sasa,na ninawajua mpaka majina yao yote ya ile familia” alisema Mwana Fa

Hata hivyo Mwana Fa anasema kuwa anazidi kumpongeza Diamond kwa sababu alichokifanya katika huu wimbo umemfanya kuwa tofauti na vile mashabiki wake walivyomzoea maana amekuja kitofauti kabisa na inapendeza.

Kwaio niliposikia wamefanya kazi na mbongo  ilinivutia sana na hata  nilipoisikiliza ngoma ni nzuri sana.Ipo tofauti kubwa hata Miamond sio yule ambae  tumemzoea, kwaio ile ngoma ni kali sana.Mimi naona love yangu kwa MorganHeritage iko palepale na  naona wamezidi kuichukua zaidi baada ya huu wimbo na Diamond Platinumz” aliendelea kuongea Mwana Fa

MorganiHeritage ni kundi bora Duniani linalofanya vizuri kabisa katika miondoko ya raggae, na hivi karibuni walifanya kazi nzuri na msanii mmoja kutoka bongo Diamond Platinumz.Wasanii kama Mwana Fa ni watu wanaonyesha mfano bora pale wanapoona wasanii wenzao wamepatia hawajifichi kuonyesha hisia zao kwa jambo ilo, kitendo alichokifanya mwana fa ni kuonyesha upendo kwa msanii  mwenzie.

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.