Mwana FA Ampa Shavu Jay Dee Kwenye Wimbo Wake Mpya

Ni ya kama miaka mitano imepita tangu wasanii wakongwe wa muziki wa Bongo fleva nchini, mwanadada Lady Jay Dee na Mwana FA  walipofanya kazi ya pamoja ilikuwa ikijulikana kama “Hawajui’, kazi ambayo ilifanya vizuri sana kama muziki wa bongo, wasanii hao ni  kati ya wasanii wa kwanza na wakongwe kabisa waliwahi kuafanya vizuri na wanaendelea kufanya vizuri mpaka sasa katika tasnia hii ya muziki.Hata hivyo kuna kiprind kirefu kimepita ambapo wasanii hawa wawili walikuwa wakionekana katika bifu zito ilhali hakukuwa na sababu ya wazi kwa bifu lililokuwa likiendelea kati yao, kiasi kwamba walishindwa hata kuendelea kufanua kazi pamoja.

Hivi juzijuzi msanii wa kike Lady Jay Dee alitoa wimbo wake mpya wa” I miss you’, ambao kwa sasa unafanya vizuri katika vituo mbalimbali  vya Radio na Televisheni, lakini jambo la kufurahisha zaidi ni pale msanii Mwana FA alipoamua kupost katika ukurasa wake wa Instagaram na kuonyesha support  kwa msanii huyo wa kike kwa kutoa wimbo wake mpya,akiwa kama msanii mkubwa na anaependwa ma kufuatwa na watu wengi nchini na hata Duniani, Mwana FA kupost kazi ya Lady Jay Dee ianongeza idadi ya mashabiki hata kwa Lady Jay Dee pia na ni njia moja kubwa na nzuri ya kufanya wimbo wake mpya uendelee kujulikana na watu wengi zaidi.

download latest music    

Post ya Mwana FA kwa Lady Jay Dee

Sio hivyo, lakini jambo kubwa zaidi hii inaonyesha kuwa kumbe wawili hao walishamaliza tofauti zao na wamefikia hatua nzuri ya kuanza kusaidiana tena katika muziki.Hata hivyo baada ya kupostiwa kwa wimbo huo katika ukurasa wa Mwana FA naLady Jay Dee alijibu kwa kuandika “more blessings

Ukiachilia mbali na Mwana FL wasanii wengine walionekana kufurahishwa na ujio mpya wa lady Jay Dee n pamoja na Proffessa Jay, pamoja na msanii AY.Hata hivyo mashabiki wengi wameonekana kufurahishwa na hatua kubwa ya wasanii hawa kuonekana kuwa pamoja tena na kumaliza tofauti zao ili waweze kuendelea kufanya kazi pamoja hatimaye kukuza muziki wa tanzania ilhali wao ni wasanii wakongwe kabisa katika muziki.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.