Mzee Yusuph- Maisha Ni Magumu Tangu Nimeacha Muziki

Aliyekuwa Mwanamuziki wa nyimbo za taarab nchini Mzee Yusuph amefunguka na kuelezea hali yake ya kiuchumi ilivyo ngumu tangu aache kuimba.

Mzee Yusuph alijizolea umaarufu katika sanaa hiyo baada ya kuonyesha umahiri mkubwa na kuopngoza bendi  yake ya Jahazi Modern Taarab.

download latest music    

Siku za nyuma kidogo Mzee Yusuph alitangaza kuachana rasmi na muziki wa Taarab kwa sababu za kidini na kuamua kuachana na mambo ya kidunia na badala yake kumgeukia Mwenyezi Mungu.

Hivi sasa Mzeee Yusuph anafunguka na kueleza jinsi maisha yanavyomuwia ugumu tangu alipoachana na sanaa hiyo.

Kwenye mahojiano aliyofanya hivi karibuni Mzee Yusuph alifunguka haya:

Tangu niache kufanya Muziki wa kidunia kipato changu kimeshuka sana sasa hivi nafanya biashara ya kuuza matofali ila uzalishaji ni mdogo kutokana na kwamba mtaji ni mdogo ila pia kuna changamoto za hapa na pale sahivi kuna mvua na nini”.

Tangu Mzee Yusuph aachane kufanya Muziki inasemekana kuwa muziki huo umeishia kuzorota na hata kufa kabisa.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.