Mziki Wa Bongo Fleva Unakufa Kwasababu Ya Wasanii Kupenda Kiki- Ney Wa Mitego

Mwanamuziki wa Bongo fleva, Ney Wa Mitego amefunguka na kuamua kuwachana wanamuziki wenzake wote anaodai kuwa wanapenda kutafuta kiki kuliko kufanya mziki unaoeleweka.

Ney Wa Mitego alitumia mtandao wa kijamii kufikisha ujumbe wake ambao alidai wasanii wa bongo fleva kupenda kutafuta kiki kunapelekea kuua mziki kwani kiki inakuwa kubwa na mziki unakuwa wa kiwango cha chini sana kupita promo uliopata.

download latest music    

Ney Wa Mitego alifunguka:

Wasanii wenzangu kusema kweli kuna kitu nakiona kwenye gemu yetu, kwenye mziki wetu wa bongo fleva tuna kibarua kikubwa cha kurudisha mziki kwenye mstari ulionyooka kwa sababu imefika time watu sasa hivi wanatengeneza kiki kubwa alafu mziki mdogo, yaani kiki zimekuwa mbele mziki uko nyuma unasindikiza, tukiendelea hivi miaka miwili mitatu ijayo naiona bongo fleva ikiwa imepotea kama bongo movie ambavyo imepotea, Kama tusipokuwa makini kuamua kufanya kazi na mini viwe ni vitu vya kusindikiza mziki, sahivi mambo yamebadilika imefika time watu wanatengeneza kiki ambazo yaani hazielezeki alafu mziki unachukua nafasi ndogo sana unasindikiza kiki jamanii ehee tunajisahau tuamke turudishe mziki wetu kwa sababu tunakuwa tunawalemaza sana mashabiki zetu”.

Wasanii wengi wa Bongo fleva siku hizi wamekuwa na kawaida ya kutengeneza kitu kinachoitwa kiki yaani wanajitengenezea  skendo kubwa kwenye mitandao ya kijamii mara tu pale wanapokaribia kutoa nyimbo mpya ili tu wawe wanazungumziwa kipindi nyimbo inatoka kwa madai kazi inapata promo kubwa na ushabiki mkubwa.

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.