Nai Adai Kumwacha Moni Kisa Michepuko

Mwanadada mrembo ambaye ni Model wa Instagram na make up Artist Nai Officiall amefunguka na kusema amembwaga aliyekuwa mpenzi wake rapa Moni Centrozone kisa michepuko.

Moni na Nai enzi za Mapenzi yao

Moni na Nai walikuwa Kwenye Mahusiano ya muda mrefu lakini sasa anaweka wazi kuwa Hawapo pamoja Tena kwani ameshachoshwa na Michepuko ya mwanaume huyo.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Enews ya East Africa Tv, Nai amesema ameshamfumani Moni na mwanamke mwingine ingawa yeye anakataa na hata kuna Michepuko inapiga simu yake ovyo:

Nimeshagombana naye sio chini ya mara nne na mara ya mwisho tumegombana mpaka nikataka kuondoka nilikuwa nimekasirika nikamwambia mimi siwezi kuendekea na wewe we siunaona huyo mwanamke mwingine wa muhimu?

Lakini pia kuna mwanamke mwingine alikuwa Anatembea naye mtaani nikathibitisha nikamfuata yule mwanamke akaniambia sitembei na bwana ako ila bwana ako ndio ananitaka basi tukaishia kugombana nikaondoka nikarudi kwetu”.

Wikiendi iliyopita Moni alimtuhumu Nai kwa kumkimbia baada ya ya kupata ajali na kumuua mguu kitu ambacho Nai amekataa na kudai sababu pekee iliyomfanya aondoke ni baada ya kuona Moni kaenda kutembelewa hospitali na mchepuko wake.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.