Napenda Wanawake Natural, Hamtomuona Mke Wangu na Make-up

Rapa wa muziki wa Bongo fleva kutoka katika kundi la Weusi, Nikki wa pili amefunguka na kuweka wazi kuwa anapendelea kuwa na mwanamke ambaye hajirembi ‘natural’ hivyo msitegemee kumuona mke wake na make-up.

Niki wa pili amekuwa akimposti sana mpenzi wake Kwenye ukuras wake wa Instagram ambapo msichana huyo huoneka akiwa natural sana habari mawigi, anabana tu nywele zake lakini pia hapaki make up sana.

download latest music    

Wiki iliyopita Dogo Janja alimchana Niki na kumwambia mwanamke make up natural aiachie misitu comment ambayo ili trend sana lakini sasa Niki wa pili an Afunguka kuhusu kauli yake ya kupenda mwanamke ambaye hapaki make up.

Kwenye Interview aliyofanya na Enews ya East Africa Tv Nikki wa pili alifunguka na kuweka wazi mke wake hatokaa apake make up:

Hakuna kitu kizuri kama mwanamke ambaye yupo asilia natural kwani sisi binadamu ni wazuri kwa sababu ni asili  na mara nyingi ukibadilisha asili unakuwa unaiharibu na mimi naamini uzuri wa msichana upo kwenye asili yake hivyo msitegeemee kumuona amepaka make up labda lipstick kidogo”.

Niki wa pili amekuwa Kwenye Mahusiano na mrembo huyo ambaye ni mwanafunzi wa chuo kikuu cha Dar es Salaam kwa kipindi kirefu kidogo.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.