Napitia Changamoto Nyingi Lakini Napambana- Rich Mavoko

Mwanamuziki mkongwe wa muziki wa Bongo fleva Richard Mavoko ‘Rich Mavoko’ amefunguka na kuweka wazi kuwa amekuwa akipitia Changamoto nyingi kwenye Safari yake ya muziki.

Mavoko amesema katika Safari yake nzima ya muziki tangu ameanza miaka ya nyuma amekuwa mtu wa kukatishwa tamaa katika kila hatua anayofika.

download latest music    

Mavoko aliyejitoa katika kundi la WCB hivi karibuni alisema maisha yake ya muziki yamepitia vikwazo vingi kufika alipo lakini hawezi kukata tamaa na atahakikisha anapigana na kuufikisha muziki wake mbali.

Mimi ni moja ya vijana tuliopitia changamoto nyingi kwenye kazi zetu, lakini napambana kuhakikisha kipaji changu kinazidi kupaa ndani na nje ya nchi“.

Hivi karibuni Mavoko aliwanyooshea kidole WCB kwa kutumia mbinu mbali mbali ili kumzibia riziki katika kufanya muziki Wake .

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.