Natafuta Mwanaume Ambaye Atakuwa Baba Kwa Watoto Wangu-Zari

Mfanyabiashara maarufu Zarinah Hassan ‘Zari The Bosslady’ na mzazi mwenzake na staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz amefunguka na kuweka wazi tangu ameachana na Diamond amekuwa akitafuta mwanaume ambaye atakuwa kama baba kwa Watoto Wake.

Baada ya mahusiano ya takribani miaka minne Zari alimtosa Baba Watoto Wake Diamond mapema mwaka huu katika siku ya wapendanao tena kupitia ukurasa wake wa Instagram.

download latest music    

Sasa Zari ameweka wazi kuwa tangu aachane na Diamond  ameshakuwa na mahusiano na wanaume kadhaa lakini hivi sasa anataka mwanaume ambaye atakuwa mfano bora wa baba kwa  watoto wake wa kiume na mwanaume ambaye binti yake wa kipekee atatamani kuwa mfano wa mwanaume wa kuolewa naye.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Zari ameandika maneno haya:

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.