“Natamani Shilole Awe Swala Tano Kama Uchebe”- Rey Jones

Mrembo aliyewahi kuwa Meneja wa wasanii mbali mbali wa Bongo fleva kama vile Maua Sama, Msami baby pamoja na Dito huku akifanya kazi kwa karibu pamoja na wasanii wengine kama Shilole na wasanii wengine.

Rey Jones ambaye ni maarufu kama chui jike amesema anatamani sana rafiki yake Shilole awe mtu wa swala tano kama mume wake Uchebe.

download latest music    

Rey Jones amesema ingawa Shilole ni muislamu mzuri tu tayari lakini anatamani awe kama uchebe ambaye hakosi swala tano kwa siku.

Msanii maarufu Bongo Shilole aliuaga ukapera mwaka jana mwishoni baada ya kufunga ndoa ya siri na mume wake wa hivi sasa Uchebe ambaye ni swala tano na ameshika sana dini.

Rey Jones alimpa ushauri huo Shilole kwenye interview aliyofanya na kituo cha Dizzim Online ambpo alifunguka yafuatayo:

Uchebe ni mtu wa dini dini sana natamani na Shilole nimuone kwenye upande huo ingawa ndio yupo huko tayari lakini ana utofauti na mumewe maana Uchebe ni wale wanaitwa swala tano ile yaani kwa siku hakosi hata moja ila shishi Kama anapiga basi itakuwa moja anagusa gusa yaani mimi nataka aanze kuzipiga zote”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.