Navy Kenzo Wafungukia Tetesi Za Kijamii WCB

Kundi la muziki la Navy Kenzo linaloundwa na wasanii  ambao ni Producer na msanii Nahreel na mpenzi wake Aikah limefungukia tetesi zilizosambaa Kwenye mitandao ya kijamii kuwa wamesiniwa na lebo ya WCB.

Navy Kenzo walitengeneza headlines wiki iliyopita baada ya kutotoa ngoma kali waliomshirikisha Diamond lakini baadae kuna tetesi zilisambaa kuwa kundi hilo linasiniwa na linakuwa chini ya WCB.

download latest music    

Tetesi hizo zilishika kasi mara baada ya Harmonize kuandika kwenye ukurasa wake wa Instagram kuwa anawakaribisha kundi hilo katika Label ya WCB na Nahreel alionekana kukubaliana na Harmonize.

Lakini Navy Kenzo wamekanusha taarifa hizo na kuweka wazi kuwa wenyewe wako chini ya Meneja Salaam SK ambaye pia ni Meneja wa Diamond lakini sio chini ya WCB na kama siku wakijiunga WCB tamko litatoka rasmi kwao.

Navy Kenzo wanafanya vyema sana na wimbo wao mpya wa ‘Katika’ waliomshirikisha Diamond Platnumz ambao mpaka hivi sasa wanashikilia nafasi ya kwanza katika kutrend Kwenye Media mbali mbali.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.