Navy Kenzo Wagoma Kufanya Kazi na WCB
Wasanii wanaounda kundi la Navykenz wakiwa ni wapenzi wa muda mrefu Aika na Nahrelly wamekanusha taarifa za wao kujiunga na lebo ya Wasafi.
Wakiwa kwenye mahojiano walipoulizwa kuhusu tetesi zinazosambaa za wao kujiunga na lebo ya wasafi walijibu kuwa „hatujajiunga na lebo ya wasafi sisi tuko chini ya Manager Sallam SK ndie anasimamia kazi zetu hizo habari za mitandao sio za kweli”
Story za Navkenzo kujiunga Usafini zilienea baada ya kundi hilo kutoa ngoma iitwayo ‘katika’ ambayo wamemshirikisha Diamond Platnumz, ngoma ambayo kwa sasa imekuwa gumzo katika mitaa mbali mbali.