NavyKenzo Kutoa Shilingi Milioni Mbili Kwa Shabiki Mmoja

Kikundi cha muziki wa Bongo fleva cha NavyKenzo kinachoundwa na wasanii wawili ambao ni Nahreel na Aikah wamekuja na zawadi ya pesa taslimu kwa ajili ya mashabiki zao.

NavyKenzo wametangaza zawadi hiyo nono baada ya kuachia ngoma yao mpya inayoitwa ‘Fella’ ambapo shabiki atajinyakulia kitita hicho cha pesa kama atacheza wimbo huo.

download latest music    

NavyKenzo wametangaza zawadi hiyo nono Kupitia ukurasa wake wa Instagram ambapo wameandika:

Fella Dance challenge, Winner get 1000usd, Tunatoa dola 1000 ambayo ni  sawa na milioni 2 na lakini 2 kwa mshindi tuma clip yako”.

Fella ni wimbo wa kwanza kwa Navy Kenzo kutoa mwaka huu tangu pale walipomshirikisha Patoranking katika wimbo wao unaokwenda kwa jina la Bajaj uliotoka June 19, 2017.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.