Navykenzo Watia Msisitizo Kuwa ‘Fela’ Haijabuma

Wasanii kutoka kundi la Muziki la Navykenzo Nahreel na Aikah Marealle wamekana maneno maneno yanayosemwa dhidi ya single yao mpya inayoitwa ‘Fela’ kudaiwa kubuma.

Navykenzo walitoa Fela siku chache zilizopita lakini kuna tetesi kuwapatanisha wimbo huo umebuma kwani haujapata mapokezi mazuri kutoka kwa mashabiki.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Risasi Vibes Aikah ameweka wazi kuwa wimbo wao mpya wa Fella, haujabuma bali unafanya vizuri na kipimo cha wimbo kufanya vizuri kwao si ‘views’ za Mtandao wa YouTube pekee.

Wimbo wa Fella unafanya vizuri, kwenye media mbalimbali, anayesema umebuma atakuwa si mfuatiliaji mzuri wa muziki na ‘trend’ ya muziki kwa jumla”.

Navykenzo ambao wamekuwa na kawaida ya kutoa nyimbo ambazo siku zote zimekuwa zikifanyavizuri kama vile Kamatia chini na game na nyinginezo wamesisitiza na Fela ipo kwenye kundi hilo.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.