Nay Wa Mitego Adaiwa Kuvunja Mahusiano na Nini Baada Ya Familia Yake Kutaka Ndoa

Msanii wa Muziki wa Bongo fleva Nay Wa Mitego amedaiwa kuvunja Mahusiano na mpenzi wake Nini baada ya familia ya Nini kutaka afunge ndoa na binti yao.

Shilawadu wanaripoti kuwa Nay wa Mitego na mpenzi wake Nini wamejikuta katika wakati mgumu baada ya familia ya Nini kumkalia kooni Nay na kumtaka amuoe Nini.

download latest music    

Nay na Nini wamekuwa Kwenye Mahusiano kwa muda kidogo Lakini sasa inadaiwa Familia ya Nini imekuja juu na kumtaka Nay amuoe binti yao baada ya kukaa naye nyumbani kwake.

Inadaiwa Nini alihamisha makazi yake nyumbani kwa Nay na kila Familia yake ilikuwa ikimtafuta arudi nyumbani alikuwa anagoma ndipo walipoamua kumsaka na kumtaka afunge ndoa.

Lakini inasemekana kuwa Nay alikuwa anawapiga chenga kila wakimtafuta anajificha hataki kabisa kuonana na Familia ya Nini.

Siku ya leo Nay wa Mitego Kupitia ukurasa wake wa Instagram ametangaza kumtosa Nini na kudai yupo single ambapo kupitia ukurasa wake wa Instagram alisema “It’s Official I am Single”.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.