Nay wa Mitego: Babu Tale Kaiba Wazo Langu La Kuwapatanisha Diamond na Zari

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Nay Wa Mitego amemjia juu Meneja wa Diamond Platnumz, Babu Tale huku akidai yeye ndio aliyetoa wazo la kuwapatanisha Diamond na Zari.

Mwanzoni mwa wiki hii Babu Tale alifunga Safari kwenda nchini South Africa kwa ajili ya kuwapatanisha Diamond na Zari kitendo ambao Nay amekiri kuwa ni kizuri lakini amehoji kwa nini amesubiri mpaka yeye atoe wazo hilo alafu ndio na yeye aende.

download latest music    
Babu Tale Alipoenda South Africa kumuombea Diamond msamaha

Kwenye na mahojiano na Risas Mchanganyiko, Nay wa Mitego amemtolea povu hilo Babu Tale:

Suala la Babu Tale kwenda kumuombea msamaha Diamond ni zuri lakini alitakiwa afanye hivyo muda mrefu na siyo asubiri mpaka nizungumze mimi kwamba nitawapatanisha. “Nashukuru wazo langu limekubalika na kila mtu na yeye mwenyewe kuliona linafaa na kufanyia kazi.

Diamond ni mshikaji wangu wa muda mrefu sana, japo mapenzi hayaingiliwi lakini kwa upande wangu namkubali sana mama Tee (Zari) maana akiwa naye mambo yake yanakuwa kwenye mstari kwani anakuwa mtu wa kazi sana tofauti na akiwa na hawa wanawake wengine.

Kutokana na kuliona hilo ndiyo maana niliona nimpe ushauri kupitia ukurasa wangu wa Instagram na kuahidi kuwarudisha pamoja, lakini kabla sijafanya hivyo, Babu Tale akalifanyia kazi, siyo vibaya nimefurahi sana kwa kweli”.

Siku video ya wimbo wa Iyena ulipotoka Nay alimshauri Diamond aachane na Hamisa na arudiane na Zari na hata kumuhaidi atasaidia kumuombea msamaha na kuwapatanisha.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.