Nay wa Mitego: Bongo Fleva Itakufa na BASATA na Serikali Ndio Chanzo

Mwanamuziki wa Bongo fleva Nay wa Mitego amefunguka na kusema Muziki wa Bongo fleva uko mbioni kupoteza na kufanya kama Bongo fleva na hii yote inasababishwa na serikali na BASATA.

Wiki chache zilizopita Nay wa Mitego alikuwa mmoja kati ya wasanii waliofungiwa nyimbo kuchezwa kwenye vyombo vya habari kwa madai kuwa haziendani na maadili ya Tanzania.

download latest music    

Maoni hayo ya Nay wa Mitego  yalikuja baada mjadala mzito kati ya Naibu Waziri wa habari Juliana Shonza na viongozi wa BASATA walipokuwa wanajibu maswali mbali mbali kuhusu hatua wanazoendeela kuchukua dhidi ya wasanii hao.

Kwenye mjadala watu wengi waliuliza maswali kuhusiana na vigezo vya kufungiwa kwa wasanii na nyimbo zao huku wengine wakihoji kwanini BASATA wanasimamia kigezo cha maadili pekee? lakini majibu kutoka BASATA hayakuwaridhisha wala kuwaingia vichwani baadhi ya wasanii akiwemo Nay Wa Mitego.

Nay wa Mitego alitumia ukurasa wake wa Twitter na kuweka ujumbe wake huo wa kukata tamaa juu ya Bongo fleva:

Kwa mahojiano yao leo mtakua mmeelewa tatizo ni nini.?! Naona mwisho wa huu muziki, Umekwamia hapa rasmi 2018. Mkubwa atabaki kuwa mkubwa na mdogo ataendelea kuwa mdogo. Na tusivyo na umoja tunaenda walikoenda ndugu zetu Bongo Movie“.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.