Nay Wa Mitego Kumlipisha Diamond Fidia

Ikiwa bado anaendelea na kesi yake ya kutakiwa kulipa fidia kwa wasanii wakongwe nchini  wa band ya Msondo Ngoma baada ya kutumia ala yao ya sauti  Saxophone na kuweka katika wimbo wao wa Zilipendwa, hivi karibuni tena Diamond ametoa wimbo mpya ambao pia umekuwa na vionjo vya wimbo wa Ney wa Mitego unaojulikana kama makuzi ambao Diamond ametoa akimshirikisha msanii mkubwa Dunianai Rick Ross.

anaemiliki muziki huo wa makuzi ney wa mitego   anaweza kuwashitaki wasafi kwa kutumia kionjo hicho cha muziki wake bila kuwa na ruhusa yake.uongozi wa free nation ambapo ndio anapofanyia kazi ney wa mitego wana haki ya kudai fidia baada ya msanii huyo kutumia baadhi ya sehemu za wimbo wao katika wimbo mpya wa diamond.

download latest music    

Hata hivyo uongozi wa Free Nation chini ya Ney wa Mitego amesema kuwa wameamua kuwapa muda Wasafi na kujifikiria nini kufanya kabla  hawajaamua kuwapeleka mahakamani.

Hata hivyo meneja wa Diamond ,Babutale amejibu tuhuma hizo na  kusema kuwa wako tayari kukaa mezani na viongozi wa Free Nation ili kulizungumzia swala hilo hata hivyo meneja huyo alionekana kujiamini na kusema kuwa siku zote anaedaiwa huwa ni tajiri huwezi ukakuta maskini anadaiwa hata siku moja.

kumekuwa na malalamiko mengi kwa wasanii wa Tanzania kuibiwa baadhi ya maneno, mashairi au vionjo vya nyimbo zao bila kunufaika na nyiimbo hizo, Free nation hawatakuwa watu wa kwanza kutoa malalamiko , wapo wasanii wengi amabo wamekuwa na malalamiko ya aina hii.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.