Ndoa Ya Kajala Yadaiwa Kupamba Moto

Muigizaji wa Bongo movie Kajala Masanja ‘Kay’ amedaiwa kuwa mbioni kufunga ndoa hivi karibuni na kigogo mmoja wa serikalini.

Global Publishers wanaripoti kuwa Kajala yupo katika harakati za kufunga ndoa na Kigogo ambaye ana mpunga  mrefu ambapo inadaiwa Kajala kabadilisha kabisa mfumo wa maisha yake ili kujiandaa kuwa mke wa mtu.

download latest music    

Mtu wa karibu wa Kajala ametoa habari hizo kuhusu Msanii huyo na kuigungukia Global Publishers:

Kajala siku hizi kumuona ni shughuli kwa sababu muda si mrefu anaolewa na kigogo mmoja ambaye amembadilisha maisha yake. Ndiyo  maana siku hizi huwezi kumkuta akijichanganya hata kidogo kama ilivyokuwa huko nyuma.

Sasa hivi huyo kigogo anayemuoa anadai ndiye mtu anayeweza kuishi naye muda mrefu. Hata hivyo, ndoa yao hiyo bado imefanywa kuwa  siri“.

Baada ya Habari hiyo gazeti hilo lilimtafuta Kajala ili kujua ukweli wa mambo ambapo alikataa kuthibitisha au kukataa habari hizo:

Ndoa gani au unanichuria? Kwa nini mnapenda kusikiliza maneno ya waongeaji? Kama kuna mtu anataka kunioa si mtaniona ndani ya shela tu? Hilo ni jambo jema, kama lipo nitaliweka wazi siku si nyingi.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.