Ndoa ya Young Dee Yayeyuka , Kumbe Ilikuwa Kiki.
Kulikuwa na picha zilizokuwa zikisambaa katika mitandao ya kijamii zikiomyesha kuwa msanii wa bongo flev, Young Dee amefunga ndoa na mwanamke mmoja inaeemekana kuwa sio wa nchini,maswali mengi yalitanda kutokana na ukimya na usiri wa ndoa hiyo.
Hata hivyo wengi walikuja kuamini kutokana na pongezi nyingi walizokuwa wakipewa kutoka kwa watu mbalimbali kuhusu hatua aliyoichukua ya kufunga ndoa na mwanamke huyo.
Ndoa hiyo imeota mbawa baada ya kuonekana kwa video mpya ya Young Dee ya wimbo ulikwenda kwa jina la naoa ambapo picha hizo ni photoshots za wimbo huo.
Imekuwa ni jambo la kawaidia kwa wasanii kufanya kitu kikubwa kitakachowafanya mashabiki kukaa attention kumbe inakuwa ni kiki ya kutaka kutoa wimbo mpya, hiki alichofanya Young Dee pia walishafanya watu wengi katika game.