Nedy Music Adai Ataoa Wanawake Wanne

Msanii wa Muziki wa Bongo fleva anayefanya vyema na wimbo wake wa ‘Homa Ya Jiji’ Nedy Music amefunguka na kuweka wazi mipango yake ya kuoa wanawake wanne katika siku za mbeleni.

Lakini pia Nedy amedai kwa yeye kama Muislamu anaruhusiwa kuoa idadi hiyo ya Wanawake Lakini pia amedai anataka kuzaa watoto wengi kadri atakavyoweza hata ishirini.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Bongo 5, Nedy Music amefunguka haya:

Mimi Baba yangu alioa wanawake wanne hata kwangu kama nitajaliwa riziki ya kutosha basi nitaoa wanawake wanne panapo majaaliwa na hata watoto nataka kuwa na hata timu inshallah na hata wakifika ishirini mimi ninao uwezo wa kuwaandaa”.

Lakini pia Nedy Music amemkingia kifua Ommy Dimpoz na kumtetea dhidi ya tuhuma kuwa ametafuta kiki kwa kusambaza taarifa kuwa yupo ICU na kusema Ommy hawezi kufanya kitu kama hiko maana sio mtu wa kiki.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.