Nedy Music Adaiwa Kumtosa Ommy Dimpoz

Mwanamuziki wa Bongo fleva Nedy music amefungukia tuhuma na maneno yanayondelea Kwenye mitandao ya kijamii kuwa amemtosa Staa wa Bongo fleva Ommy Dimpoz.

Nedy Music alianza sanaa yake ya muziki akiwa kama msanii anayejitegemea kutokana na kipaji chake alichukuliwa na Ommy Dimpoz na kusainiwa chini ya label ya Pozi kwa Pozi (PKP).

download latest music    

Lakini baadae Ommy Dimpoz na yeye alienda akasainiwa chini ya label ya Alikiba Rock star 4000 na tangia hapo kukawa na tetesi kuwa Nedy Music amejitoa PKP.

Lakini pia tetesi hizo zilizidi kushika kasi Siku mbili hizi baada ya Nedy Music kutoa wimbo wake mpya aliomshirikisha Ruby na kwenye video hiyo hapakuonekana logo ya PKP hivyo kusemekana amejitoa PKP.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Enews Nedy Music amefunguka na kukataa tuhuma hizo na kuweka wazi kuwa bado yuko PKP:

Mimi najibu kuwa nipo PKP bado sijatoka na CEO ni Ommy dimpoz na PKP bado tupo kama kawaida.

Naomba Mashabiki waendelee kusapoti kazi zangu maana nafanya kwa ajili yao kwaiyo wasiniangushe wanipe tu sapoti ya kutosha”.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.