Nedy Music Afungukia Hali Ya Kiafya Ya Ommy Dimpoz

Msanii wa Bongo fleva anayefanya vizuri katika Tasnia hii ya Bongo fleva amefunguka hali yake ilivyo kwa sasa kutokana na kuumwa kwa Msanii mwenzake Ommy Dimpoz.

Wiki chache zilizopita Ommy Dimpoz alitangaza kwa mara ya kwanza kuwa alikuwa hoi hospitalini akiwa amelazwa baada ya kufanyiwa operesheni Kwenye shingo.

download latest music    

Ommy Dimpoz aliweka wazi kuwa tangia kipindi kile hali yake ilikuwa imeanza kuimarika kwa kiasi kikubwa.

Nedy Music ni mmoja kati ya wasanii waliopo chini ya label ya Ommy Dimpoz inayoitwa PKP Entertainment na amefunguka hali ilivyo tangu Ommy Dimpoz aanze kuugua.

Kwenye mahojiano na Clouds FM, Nedy Music amekiri kuwa  kipindi hiki ambacho Dimpoz anaumwa kuna vingi anavikosa kutoka kwake.

Kuna vitu vingi ambavyo navimisi kutoka kwa Ommy Dimpoz haswa kipindi hiki anachoumwa. Ni mtu ambaye ananishauri mambo mengi, na mara nyingi huwa tunakaa na kusikiliza kazi zetu”.

Ommy Dimpoz bado yuko nchini Afrika ya Kusini kwa ajili ya matibabu zaidi.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.