Nedy Music Afungukia Mipango Ya Kolabo na Vanessa Mdee

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Nedy Music amefunguka na kuweka wazi mipango yake ya kufanya kolabo na msanii mwenzake wa Bongo fleva Vanessa Mdee ‘Vee Money’.

Nedy Music ambaye amekamata headlines kwa siku kadhaa sasa Baada ya kujishindia tuzo za Afrimma zilizofanyika nchini Ghana ameweka wazi Kama ana mpango wa kufanya kolabo na Vanessa Mdee.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na kipindi cha The Playlist cha Times Fm, Nedy Music amesema si kweli kwamba walifanya kolabo nchini Ghana walipokutana Kama tetesi zinavyosambaa kwenye mitandao ya kijamii hivi sasa.

Hapana sijafanya kolabo na Vanessa Mdee nchini Ghana na kama kutakuwa na kolabo itafanyika nchini Tanzania”.

Nedy Music na Vanessa Mdee walikutana na nchini Ghana ambako wote wawili walikuwa wamechaguliw kushiriki tuzo hizo lakini Vanessa hakuweza kupata tuzo hizo na Nedy alifanikiwa kijinyakulia tuzo moja.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.